Kitabu/Kitini hiki ni Mwongozo wa Mafunzo ya Kilimo Hifadhi kwa Wakulima, Viongozi na Maafisa Ugani. Pia ni kwa ajili ya kufundishia wakulima wengine wa vijijini kuhusu Kilimo Hifadhi. Mwongozo huu hautoi maelezo kwa kina juu ya Kilimo Hifadhi bali unaeleza kwa kifupi mbinu na kanuni za Kilimo Hifadhi. Kimsingi mwongozo huu ni kwa ajili ya kufundishia Wakulima, Viongozi, na Maafisa Ugani mbinu na kanuni mbali mbali za Kilimo Hifadhi ambao pia nao watatoa mafunzo haya kwa wakulima wengine huko vijijini.
...