Written by
Publisher Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo
Kilimo cha bustani kinahusika na uzalishaji wa mazao ya aina ya mboga, matunda, viungo na mimea ya mapambo. Kilimo cha bustani ni chanzo cha ajira na pato kwa wakulima na watu wengine. Mboga na matunda yanatupatia virutubisho vya kujenga, kutia nguvu na kulinda mwili. Zaidi ya hivyo, mimea ya mapambo hutumika katika kuremba na kuboresha sehemu za makazi, majengo, barabara na sehemu zingine za wazi za jumuia. Hii ni muhimu sana katika swala zima la kuhifadhi mazingira.
...