You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs
Usilolijua ni kama usiku wa giza
Join
or login
to VOTE
Votes
13
"na Ibrahim Nyanda
🏆 Shindano la Insha ya Methali
“Ni kwa nini kijiji chetu hakina maendeleo ukilinganisha na vijiji vingine vinavyotuzunguka? Vijana wengi kutoka vijiji vingine wa umri wetu wamesoma na wengine wana kazi zao za maana huko mjini. Pamoja na kwamba kuna shule kijijini kwetu lakini vijana hatufanyi vizuri shuleni na hata walimu wanapoajiriwa hawakai muda mrefu wanahama. Kuna nini hapa Bombambili?" Haya ni maswali ambayo kijana Akilimali alimwuliza rafiki yake Manase wakiwa machungani wakilisha ng’ombe. 

Mara baada ya swali hili Manase alionekana amezama katika wimbi kubwa la mawazo na mara baada ya kufikiri kwa muda alimgeukia rafiki yake Akilimali na kumtazama kwa kina kiaha akamwuliza, “Unaamini kuhusu ushirikina” Akilimali alijibu kwa kutikisa kichwa kuashiria kukubaliana na swali aliloulizwa na kisha akasema “Naamini kwani mara kadhaa nimekua nikiona watu wakienda kwa waganga na wengine wanapopitia magumu huamini wamerogwa, si unakumbuka juzi bibi Andunje tulivyoambiwa kuwa amekutwa juu ya paa la mzee Masanja uchi wa mnyama akiwanga, sasa mpaka hapo naachaje kuamini mshikaji wangu” 

Manase alimwangalia Akilimali kwa makini kisha akamwambia, "Nataka nikueleze siri moja ambayo huwezi amini……. hivi unajua kama mama yako na dada yako ni wachawi?” Akilimali alibaki ameduwaa mithili ya mjusi aloyebanwa na mlango halafu akiwa amefura kwa hasira akamwambia Manase “Aisee mwanangu usianze kuniletea habari zako za udwanzi hapa, tena koma kabisa kumwambia mama yangu mchawi vinginevyo ntakuja kukufanyia kitu mbaya hutokuja kuamini macho yako, ohoooo!!” 

Manase alimtuliza rafiki ake Akilimali halafu akamwambia, “Ngoja niwarudishe ng’ombe jirani afu nikupe mchapo mzima ulivyo, najua utanielewa we punguza jaziba kwanza” 

Mara baada ya kurudisha mifugo jirani Manase akaanza kumweleza Akilimali, “Rafiki angu nataka nikupe siri hii ambayo nimekaa nayo kwa muda mrefu, chochote unachokiona hapa hata kutokuwepo kwa naendeleo kijijini ni kwa sababu ya ushirikina, kila siku mama yako na dada yako huwa ninawaona wakija nyumbani wamepanda fisi wakimpitia mama kwenda kuwanga…..” Manase alitulia kidogo halafu akaendelea 

“Huwezi kuamini kwani hata mimj nilikua siamini mpaka nilipopakwa dawa na kuwaona, nitakupa hiyo dawa utapaka machoni na utakuja kunipa majibu kesho.” 

Mara baada ya mlo wa usiku Akilimali alikua ameketi akiota moto nje ya nyumba yao ya udongo iliyoezekwa kwa nyasi wakati huo mama yake na dada yake wakiwa ndani na yeye akiwa na baba yake pale nje. Alipaka ile dawa kama alivyoelekezwa na baada ya dakika kumi alimwona dada yake na mama yake wamepanda juu ya fisi mithili ya pikipiki tayari kwa safari ya kwenda kuwanga. 

“Nisamehe sana rafiki angu, ilikua ni hasira tu” aliongea maneno haya Akilimali huku akilengwa na machozi, 

“Mimi nilijua, sasa unavyoona kijijj chetu hakiendelei hata mama yako pia na dada yako wanahusika, inaumiza sana kila mwanakijiji anayetaka kuleta maendeleo anaishia kufa, lazima kuna siku watakuja kuumbuka kama ilivyokua kwa bibi Andunje” 

“Nina uhakika hata baba yako hajui kama mama yako na dada yako ni wachawi na kila siku huwa wanaenda kuwanga na ninyi kuwaachia mauzauza mkijua wapo, nenda kampake baba yako hiyo dawa alafu utanipa majibu” alieleza Manase 

Jioni kwa siri Akilimali alimweleza baba yake kuwa dada yake na mama yake ni wachawi kitu ambacho alipinga vikali. 

“Mama leo baba anatuona, angalia anvyotutumbulia macho” dada yake na Akilimali alimwabia mama yake wakiwa juu ya fisi kama ilivyo ada wakati baba yake na kaka yake wakiwa nje wanaota moto kama ilivyo kawaida yao. 

“Sidhani kama anatuona, hebu geuza fisi tuwe kama tunawaelekea wao” ailisema mana yake na Akilimali.

Akilimali anasema hiyo ndiyo ilikua siku ya mwisho kumwona baba yake kwani baada ya kuona fisi aliyewabeba mke wake na binti yake alitimua mbio kama anashundana mashindano ya mbio za mita mia. Ama kweli usilolijua ni kama usiku wa giza, Akilimali alibaki haamini kama kwa muda wote huo ameishi na mama yake na dada yake bila kujua kuwa ni wachawi. 
Sources

Chimbuko:

Methali ya kiswahili kutoka kitabu cha “METHALI ZETU” cha Oxford inayosema “USILOLIJUA NI KAMA USIKU WA GIZA.”  

Juu ya Insha hii

Insha hii ilishika nafasi ya nne katika Shindano la Methali ya Insha la Maktaba.org 🏆 7/7/2023
Ibrahim Methusela Nyanda ni Mtanzania 🇹🇿 

Hakimiliki

Creative Commons Attribution (CC BY 4.0)
na Ibrahim Nyanda
Ilichapishwa na Maktaba.org
Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
It’s a simple and profound truth about human relationships: Making a promise means creating an expectation in others. When we fail to keep our promises, we damage our relationships and our reputation. Next time you make a promise, ask yourself, "Would I sign a contract that said this?"

French
Chose promise, chose due 
A thing promised is a thing owed. 
Russian:
Долг платежом красен, а займы отдачею. 
The beauty of a debt is its payment 
Alternative translation: A debt is beautiful when it is paid off, and loans when repaid.
Latin:
Pacta sunt servanda
Agreements must be kept (an important principle of international law)
Chinese
口說無憑
Spoken words are no guarantee.
English
Your word is your bond

What do you think? Is a promise as strong as a contract?
...
Updated 4mo ago
by

Question: Have you learned more from you parents or from your experiences in the world? 


Today's proverb is often used in Swahili to describe a person who makes a mistake that could have been foreseen and suffers negative consequences... like the truck driver in this picture from Oxfordshire, UK. Regardless of what your parents taught you (or failed to teach you), you will eventually have to confront the harsh realities of life and learn from experience.
See also: If a child cries for a razor, give it to him (Mtoto akilia wembe, mpe)

He who is not taught by his parents is taught by the world. (Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na ulimwengu)
Here's a poem by the poet Akilimali Snow-White about this proverb. (My translation from the original Swahili)

In the age they fooled me, my old folks in raising me,
I failed to learn the new movements of the world.
Today I please myself, to the people of the world, listen:
He who is not taught by his parents, is taught by the world.

I couldn’t have done any work without humbling myself before them,
Obeying to flatter them, then to serve them,
Even when I pleased them, they taught me with intention,
He who is not taught by his parents, is taught by the world.

Now I can speak European languages without difficulty,
like English and others too,
With effort I learn, and even they have raised me.
He who is not taught by his parents, is taught by the world.

I can converse without blemish,
And lead amidst evil, removing the blemish,
In the end the place pleases, one step towards harmony,
He who is not taught by his parents, is taught by the world.

There is nowhere I have overlooked, without investigation,
All sides examined, knowledge I have taken,
I even know how to sell products and buy,
He who is not taught by his parents, is taught by the world.

The amount which I have learned, not a little by fumbling,
I am pleasing where I come from, I employ good work
It’s hard to scorn, how it raises me,
He who is not taught by his parents, is taught by the world.

It’s not right to ignore what you don’t know
Try to investigate, and then analyze,
When your intention is tightened, you can’t fail to know a thing,
He who is not taught by his parents, is taught by the world.

The tasks I taught myself, my father didn’t know
He didn’t know English, or selling and buying,
but only praising oneself, that was when I, the child, knew,
He who is not taught by his parents, is taught by the world. 

I give more for you, you all who helped me,
All of you who’ve taught me, Lord give you health
God fill you all with happiness, and return goodness to you,
He who is not taught by his parents, is taught by the people of the world.
- Diwani ya Akilimali

What do you think about this poem? What does it mean? Can you improve the translation?

Fikeni E. M. K. Senkoro (1988) wrote of this poem (my translation):
[A] person can't experience everything in life from their parents: they must be ready to be taught by the world-- that is to learn from others beyond their father and mother.

...
Updated 4mo ago
by

Je, una ndoto kubwa?

Ndoto ambayo huwezi kuitimiza peke yako? Labda hata ambayo haiwezi kukamilika katika kizazi kimoja?

Kuna makanisa ya kigothi barani Ulaya ambayo yalichukua zaidi ya miaka 600 -- zaidi ya vizazi 20 -- ili kukamilisha ujenzi!

Ingawa Piramidi kubwa zaidi ya Giza imejengwa kwa kasi (ndani ya kizazi kimoja), ila pia ilichukua makumi ya maelfu ya watu.

Nchini Tanzania, Msikiti Mkuu wa Kilwa Kisiwani ulijengwa katika karne za 11-14, ukajengwa upya baada ya tetemeko la ardhi, na uliendelea kufanyiwa ukarabati hadi karne ya 18. Ulitajwa pia miaka ya 1300 na msafiri Ibn Battuta. (Je ulijua unaweza kuona Kilwa Kisiwani kupitia "ziara ya mtandaoni" yaani 3D Virtual Tour? Ona kiungo chini kwenye "Rasilimali")

Maajabu ya dunia, ya kisasa na ya kale, yalianza kama ndoto kubwa, ndoto ambazo zilichukua vizazi vingi kutimiza. Kila kizazi kiliendeleza kazi ya zamani na pia walitoa mchango wao kwa kubadilisha mipango ya siku zijazo. 

Hivyo bhasi, kama unajaribu kufanya jambo kubwa -- jambo ambalo hakika litabadilisha ulimwengu - usitarajie litafanyika kwa siku moja. Na usijaribu kuijenga peke yako. 

Methali Zinazohusiana:


 Kiswahili:
Ukitaka kwenda haraka, nenda peke yako, ukitaka kwenda mbali, nenda na wenzako

Kifaransa:
Rome ne fu[t] pas faite toute en un jour
Kutoka kitabu cha Li Proverbe au Vilain kilichochapishwa takriban mwaka wa 1190
Kifaransa cha kisasa: Rome ne s'est pas faite en un jour
Maana yake: Roma haikujengwa kwa siku moja

Kichina:
冰凍三尺,非一日之寒
Mita ya barafu sio kwa sababu ya siku moja ya baridi

Kigaelic
Chan ann leis a’ chiad bhuille a thuiteas a’ chraobh
Sio pigo la kwanza linaloangusha mti
...

Picha: Shukran kwa Zamani Project waliounda ziara ya mtandaoni ya Kilwa Kisiwani!

Updated 4mo ago
by
Kila kazi kubwa katika maisha huhitaji kufanyika kwa hatua ndogo, siku baada ya siku. 

Je, unajua methali zingine zinazofanana na hii au zinazotoa dhana hiyohiyo? 

Msemo huu unakumbusha shairi liitwalo "Vitu Vidogo" na Julia Abigail Fletcher Carney: 
Matone madogo ya maji,
Chembe kidogo za mchanga, 
hutengeneza bahari kubwa
Na ardhi ya kupendeza

Vivyo hivyo zile dakika ndogo,
ingawa ni ndogo,
hutengeneza enzi za milele. 
Julia Carney alitunga shairi hili mwaka wa 1845 darasani akiwa mwanafunzi darasani -- na alipewa dakika 10 tu kuliandika!
...
Updated 4mo ago
by