Publisher Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
MASWALI YANAYO ULIZWA KUHUSU VVU
NA UKIMWI
Virusi vya UKIMWI (VVU) ni nini? Ni virusi vinavyo shambulia kinga ya mwili na kusababisha ugonjwa wa UKIMWI.
UKIMWI NI NINI? Neno UKIMWI ni kifupisho cha Upungufu wa Kinga Mwilini:
U - Upungufu wa
KI - Kinga
MWI - Mwilini
Kuna uhusiano gani kati ya VVU na UKIMWI? Virusi Vya UKIMWI vinapoingia katika mwili wa binadamu hushambulia chembe chembe nyeupe za damu hivyo kusababisha mwili kukosa kinga yake ya asili dhidi ya magonjwa. Mwili ukipungukiwa na kinga ya asili hushambuliwa kwa urahisi na magonjwa mbalimbali, hivyo hali hiyo huitwa UKIMWI .
Kumbuka: Virusi Vya UKIMWI ni chanzo na UKIMWI ni matokeo
...