Lengo la kielekezi hiki ni kubainisha seti sahili ya maelekezo ya mwongozo wa utekelezaji na mbinu za uwezeshaji katika kuwasiliana na watoto kwa kutumia njia shirikishi. Walengwa wa Kielekezi hiki ni mashirika, asasi na watu binafsi wa Tanzania wenye lengo la kusaidia watoto katika kuyakabili masuala yao ya msingi kupitia, kwa mfano, mambo mbalimbali yanayofanyika shuleni, katika mabaraza, kamati, vyama vya wanafunzi, au katika makundi mengine yasiyo rasmi Kielekezi hiki kimeandaliwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, jinsia na watoto, kwa msaada wa kiutaalamu kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushauriana na wadau mbalimbali wanaojishughulisha na masuala ya ushiriki wa watoto nchini.
...