Mbinu 70 za ufundishaji shirikishi za kuwahusisha na kuwahamasisha wanafunzi wa kitanzania
Kiongozi hiki ni kwa walimu wanaotaka kuleta mabadiliko maishani mwa wanafunzi wao, ukiwemo ufaulu kwenye mitihani ya kitaifa. Ni mwongozo unaofaa wenye mbinu 70 za ufundishaji unaomzingatia mwanafunzi. Kiongozi hiki kinalenga kuwasaidia walimu kuzitumia mbinu mbalimbali ili kuboresha ufundishaji wao na ujifunzaji wa wanafunzi wao.
Walimu bora hubadilisha maisha. Hushajiisha. Huhamasisha. Hujitahidi kuboresha fani yao- sanaa ya ufundishaji. Walimu bora ulimwenguni hutumia mbinu za ufundishaji na ujifunzaji zinazomzingatia mwanafunzi [LCTs] ili kuwahusisha wanafunzi wao. Walimu hawa wanaelewa mapungufu ya kufundisha kwa mhadhara [lecture] ambapo mwalimu anatawala somo zima na wanafunzi wananukuu tu, na kujibu maswali machache na kuenda nyumbani kujisomea. Mbinu za ufundishaji na ujifunzaji zinazomzingatia mwanafunzi [LCTs] zinawahamasisha wanafunzi kuzungumza kuhusu kile wanachojifunza, kujifunza kutoka kwa wenzao na kuboresha uelewa wao na ukariri wa maudhui ya somo
...