You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

New announcements
Discussions
Proverbs
Usilolijua ni kama usiku wa giza
Join
or login
to VOTE
Votes
13
"na Ibrahim Nyanda
🏆 Shindano la Insha ya Methali
“Ni kwa nini kijiji chetu hakina maendeleo ukilinganisha na vijiji vingine vinavyotuzunguka? Vijana wengi kutoka vijiji vingine wa umri wetu wamesoma na wengine wana kazi zao za maana huko mjini. Pamoja na kwamba kuna shule kijijini kwetu lakini vijana hatufanyi vizuri shuleni na hata walimu wanapoajiriwa hawakai muda mrefu wanahama. Kuna nini hapa Bombambili?" Haya ni maswali ambayo kijana Akilimali alimwuliza rafiki yake Manase wakiwa machungani wakilisha ng’ombe. 

Mara baada ya swali hili Manase alionekana amezama katika wimbi kubwa la mawazo na mara baada ya kufikiri kwa muda alimgeukia rafiki yake Akilimali na kumtazama kwa kina kiaha akamwuliza, “Unaamini kuhusu ushirikina” Akilimali alijibu kwa kutikisa kichwa kuashiria kukubaliana na swali aliloulizwa na kisha akasema “Naamini kwani mara kadhaa nimekua nikiona watu wakienda kwa waganga na wengine wanapopitia magumu huamini wamerogwa, si unakumbuka juzi bibi Andunje tulivyoambiwa kuwa amekutwa juu ya paa la mzee Masanja uchi wa mnyama akiwanga, sasa mpaka hapo naachaje kuamini mshikaji wangu” 

Manase alimwangalia Akilimali kwa makini kisha akamwambia, "Nataka nikueleze siri moja ambayo huwezi amini……. hivi unajua kama mama yako na dada yako ni wachawi?” Akilimali alibaki ameduwaa mithili ya mjusi aloyebanwa na mlango halafu akiwa amefura kwa hasira akamwambia Manase “Aisee mwanangu usianze kuniletea habari zako za udwanzi hapa, tena koma kabisa kumwambia mama yangu mchawi vinginevyo ntakuja kukufanyia kitu mbaya hutokuja kuamini macho yako, ohoooo!!” 

Manase alimtuliza rafiki ake Akilimali halafu akamwambia, “Ngoja niwarudishe ng’ombe jirani afu nikupe mchapo mzima ulivyo, najua utanielewa we punguza jaziba kwanza” 

Mara baada ya kurudisha mifugo jirani Manase akaanza kumweleza Akilimali, “Rafiki angu nataka nikupe siri hii ambayo nimekaa nayo kwa muda mrefu, chochote unachokiona hapa hata kutokuwepo kwa naendeleo kijijini ni kwa sababu ya ushirikina, kila siku mama yako na dada yako huwa ninawaona wakija nyumbani wamepanda fisi wakimpitia mama kwenda kuwanga…..” Manase alitulia kidogo halafu akaendelea 

“Huwezi kuamini kwani hata mimj nilikua siamini mpaka nilipopakwa dawa na kuwaona, nitakupa hiyo dawa utapaka machoni na utakuja kunipa majibu kesho.” 

Mara baada ya mlo wa usiku Akilimali alikua ameketi akiota moto nje ya nyumba yao ya udongo iliyoezekwa kwa nyasi wakati huo mama yake na dada yake wakiwa ndani na yeye akiwa na baba yake pale nje. Alipaka ile dawa kama alivyoelekezwa na baada ya dakika kumi alimwona dada yake na mama yake wamepanda juu ya fisi mithili ya pikipiki tayari kwa safari ya kwenda kuwanga. 

“Nisamehe sana rafiki angu, ilikua ni hasira tu” aliongea maneno haya Akilimali huku akilengwa na machozi, 

“Mimi nilijua, sasa unavyoona kijijj chetu hakiendelei hata mama yako pia na dada yako wanahusika, inaumiza sana kila mwanakijiji anayetaka kuleta maendeleo anaishia kufa, lazima kuna siku watakuja kuumbuka kama ilivyokua kwa bibi Andunje” 

“Nina uhakika hata baba yako hajui kama mama yako na dada yako ni wachawi na kila siku huwa wanaenda kuwanga na ninyi kuwaachia mauzauza mkijua wapo, nenda kampake baba yako hiyo dawa alafu utanipa majibu” alieleza Manase 

Jioni kwa siri Akilimali alimweleza baba yake kuwa dada yake na mama yake ni wachawi kitu ambacho alipinga vikali. 

“Mama leo baba anatuona, angalia anvyotutumbulia macho” dada yake na Akilimali alimwabia mama yake wakiwa juu ya fisi kama ilivyo ada wakati baba yake na kaka yake wakiwa nje wanaota moto kama ilivyo kawaida yao. 

“Sidhani kama anatuona, hebu geuza fisi tuwe kama tunawaelekea wao” ailisema mana yake na Akilimali.

Akilimali anasema hiyo ndiyo ilikua siku ya mwisho kumwona baba yake kwani baada ya kuona fisi aliyewabeba mke wake na binti yake alitimua mbio kama anashundana mashindano ya mbio za mita mia. Ama kweli usilolijua ni kama usiku wa giza, Akilimali alibaki haamini kama kwa muda wote huo ameishi na mama yake na dada yake bila kujua kuwa ni wachawi. 
Sources

Chimbuko:

Methali ya kiswahili kutoka kitabu cha “METHALI ZETU” cha Oxford inayosema “USILOLIJUA NI KAMA USIKU WA GIZA.”  

Juu ya Insha hii

Insha hii ilishika nafasi ya nne katika Shindano la Methali ya Insha la Maktaba.org 🏆 7/7/2023
Ibrahim Methusela Nyanda ni Mtanzania 🇹🇿 

Hakimiliki

Creative Commons Attribution (CC BY 4.0)
na Ibrahim Nyanda
Ilichapishwa na Maktaba.org
Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
Have you ever seen a blacksmith at work? Or maybe an artisan shaping hot glass? It's pretty incredible to watch, right? (If not, visit Shanga Foundation in Arusha or check out video links below)
In our everyday experience, glass is hard, brittle and breakable, but glass is actually made by melting sand and shaping it like liquid.

Some things in life seem unchangeable; they just will not bend. If we use all our strength, they only shatter in our hands and hurt us. But a skillful craftsman can make brittle things soft and malleable by preparing them appropriately, and taking decisive action at the right moment.

This proverb is often used to mean that you should take action quickly when an opportunity arises, so that you don't miss it. See also: There is a tide
 There is a tide in the affairs of men,
 Which, taken at the flood, leads on to fortune;
 Omitted, all the voyage of their life
 Is bound in shallows and in miseries.
- Brutus in Julius Caesar, Act 4, Scene 3 by William Shakespeare
However, it's worth noting that in the play, this advice has pretty bad consequences for Brutus, who didn't exactly sail on to fortune after this speech (read more...)

Many cultures and languages have a proverb that is very similar to "Strike while the iron is hot." It seems likely that the proverb has multiple independent origins.
Chinese: 趁熱打鐵
Thai: ตีเหล็กเมื่อแดง
Hindi: लोहा गरम हैं. मार दो हथौड़ा.
Irish: buail an t-iarann te
Swahili: Fua chuma wakati kingali moto

...

Image: Elimu Yetu teachers visit to Shanga Foundation, Arusha, Tanzania

Updated 4mo ago
by
This proverb means that there are some things you can't do alone. The tango is dance for two people, so you can't dance the tango alone.

The proverb comes from a 1952 song It Takes Two to Tango:
You can sail in a ship by yourself,
Take a nap or a nip by yourself.
You can get into debt on your own.
There are lots of things that you can do alone.
But it takes two to tango, two to tango...
- It Takes Two to Tango (1952, Al Hoffman, Dick Manning and Pearl Bailey) - Check out the sources to listen to the original recording!

This proverb has many different meanings that you can apply in your daily life and relationships.  There are lots of things in life that require more than one person: It takes two people to cooperate, to make a bargain or to engage in a fight. You may really want to dance with someone, but if they don't want to dance with you, it's better to move on.  Similarly, if you're in a fight, consider how your own behavior might be contributing to continuing the fight. A dance isn't about being perfect, it's about being in time with your partner and enjoying the experience. 

Similar proverbs from Africa:
Egyptian (Arabic):
ايد لوحدها ماتسقفش‎
One hand can't clap

Swahili:
Bila mtu wa pili ugomvi hauanzi
Without a second person a quarrel cannot start

Kidole kimoja hakiuwi chawa
One finger doesn't kill a louse

...
Updated 4mo ago
by
What one person throws away may be useful and valuable to someone else.

This saying is often used to describe either the diversity of human preferences or to express optimism that humans are quite creative when it comes to repurposing or recycling what other people throw away.

For example, entrepreneur Gibson Kiwago, founder of WAGA Tanzania, recycles old laptop batteries to power homes and businesses in Tanzanzia. Check out our E-Waste Reading List!

The notion that people subjectively assess quality has been around a long time. The saying derives from a 17th century proverb:
One man's meat is another man's poison.

Have you ever seen value in something that someone else threw away?
...
Updated 4mo ago
by
by Magreth Lazaro Mafie 🇹🇿
🏆 Proverb Essay Contest 
🥉 Third Place Winner
(English translation from Kiswahili)
How many times have you heard “Mchumia juani hulia kivulini” (One who works in the sun, eats in the shade). This is a Swahili (Bantu) proverb meant to encourage people in their everyday activities, to have faith that there will be a day when they will enjoy the fruits of their work.

This proverb gives people strength, diligence, heart, courage, hope and skill in working. The worker believes that hard work brings a good harvest that will allow him to relax in the shade as he eats the fruits of his labor. 

The following poem shows “One who works in the sun” in their daily responsibilities.
I fear neither sun nor rain, making my tomorrow
I fear neither injuries nor pain, because all are temporary
Scorching sun and work are my custom, so that happiness comes in life
The street vendor, the farmer, the [port boys] and their fisherman and the sun, in search of tomorrow
One who works in the sun, eats in the shade, I am still searching for shade.

It's noon, the sun overhead, in my head I have the harvest, sweat is dripping,
The sun has set now, the oar on the beach, exhausted in bed, nets in the sea,
At home on fourth street, captain of the family, may I pull happiness from hard labor
Now the sun is rising, walking the path to look for a bite,
One who works in the sun, eats in the shade, I am still searching for shade.

Once there was a farmer. He spent his whole life in agriculture. Thus his times for pleasure were few. People in his village called him a skilled farmer. He built a house by selling part of his crops, he educated his children through farming.

This farmer was a diligent man, he always learned the principles of being a good farmer, so as time went by, he harvested many crops from his fields. Many people were really amazed to see the big changes in his family. He made many investments in his village, the farms, houses, and shops, and many livestock came from his farm.

Many people came to take wisdom from the skilled farmer. He always told them "One who works in the sun, eats in the shade. The hoe has given me respect in the village, me and my family. My life now is going on a path of certainty, I am in the shade, enjoying the fruits of my labor in the sun. I, the son of that skilled farmer, am proud of my upbringing, and his responsibility, because work in the sun today has made us rest and eat in the shade. The true meaning of “he who works in the sun” can be seen in actions. Your diligence is your sun and the shade is the fruit of your diligence.

This story is complemented by the story of "Mabala the Farmer" by Richard S. Mabala (1989). Mabala was a port worker then he was demoted, so he chose to return to the village of Morogoro. Mabala was careless, drunk and obstinate. Mabala went to the farm with a gallon of booze, he drank it and went to sleep, when he woke up, he called out to his wife but there was no answer except the sound of the hoe tik-tok, tik-tok.

Mabala was obstinate, he watered the fields with sugar, thinking it was fertilizer, but in the end he changed to become a skilled farmer, becoming “one who works” in the sun so that his family could eat in the shade. Do you feel that Mabala is “one who works in the sun”? In the family or in the community, what’s your image of a skilled farmer?

In conclusion, this story on the proverb "Work in the sun, eat in the shade" shows us a good vision in everything we do in our daily lives. Also proverbs like "Subira yavuta kheri” (Patience brings blessings), "Mgaa na Upwa hali wali mkavu” (He who combs the beach at low tide doesn’t eat dry rice) all have similar themes; they exist to give the community strength and hope each task undertaken to pursue their goals.

...
Updated 4mo ago
by