You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs

Hunger is the best sauce

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
1
Updated 5mo ago
by
View this proverb in Swahili
Njaa ni mchuzi bora
As the appetite increases, food tastes better.

The proverb first appeared in Miguel de Cervantes' Don Quixote, published in 1615 (in Part II, Chapter V)

Parents often say this to their children when they are fussy eaters.
Sources
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
Je, umewahi kuona muda huenda pole pole wakati unasubiri? Lakini kwa upande mwingine, ukivutiwa na mambo mengine, m muda huenda haraka.

Kwa mfano, ukisubiri kumwona daktari, muda ni mfupi ukiangalia simu yako au kusoma gazeti, badala ya kungoja tu kusikia jina lako liitwe.

Chimbuko cha methali hii ni Benjamin Franklin kwa Poor Richard's Almanac, hata hivyo haionekani hapo. Badala yake, Franklin aliitumia katika insha juu ya 'sumaku ya wanyama' mwaka 1785. 
Nilikuwa na Njaa sana; ilikuwa imechelewa sana; "Sufuria inayotazamwa huchemka pole pole," kama Poor Richard asemavyo.
...
Updated 5mo ago
by
na Nankya Sauda 🇺🇬
Shindano la Insha ya Methali 🏆
Mshindi wa Kwanza 🥇

Maji yaliyotulia ndiyo yenye kina kirefu

Umewahi kuchukua muda na kujiuliza kwa nini wazee huwa wana busara zaidi kuliko vijana? Je, umewahi kuchukua muda wa kutafakari asili yako ulipochipuka? Ikiwa sivyo, [sasa] ni wakati mzuri wa kuanza kutafuta asili yako kwa sababu ni muhimu mtu ajue mizizi yake.
   Baada ya muda, unachukua mzigo wa kufunua asili ya watu mashuhuri wenye akili na haiba zao, utakuja kutambua kwamba wao ni introverts (yaani wakimya, wanaopenda kukaa peke yao/kujitenga) lakini ni mashuhuri. Ni muhimu uchukue muda wako, hata ukiwa bize, ujifunze kuhusu wasomi mashuhuri kama Albert Einstein, mwanasayansi mashuhuri ambaye alisema nukuu inayotuelimisha:
"Maisha tulivu ya upweke yasiobadilikaa huchochea akili na fikra bunifu."

Hii inamaanisha kwamba wakati ukiwa peke yako ni nafasi ya kujitafakari, lakini pia ni nafasi ya kutumia akili yako bunifu. Wanasema wazungumzaji wakubwa ni wanasheria wazuri, na tumeona hayo katika maisha yetu ya kila siku ambapo watu hutoa ahadi tupu, hutoa matamko ya uwongo ili kuwapendeza waliomzunguka bila kuchukua muda wa kufanya kitu kwa nia ya kutekeleza maneno yao. Kwa sababu hiyo, wengi wamepoteza imani na hawa wanaoitwa “wazungumzaji wakubwa.”
   Kwa upande mwingine, wakimya hutushangaza kwa matendo yao. Hatua zao hupangiliwa kila mara, matamanio yao ni wazi na vitendo vyao hufanyika kwa kusudi. Wapenzi wakimya hukuza mahusiano yao ya kimapenzi kwa ubunifu mpya ili kudumisha mahusiano. Waliowaajiri [wakimya] na waliokaa karibu na introverts husema kuwafahamu ni moja ya mafanikio makubwa katika maisha yao, ndo maana hawa wamefanya kazi nadhifu zaidi, wakawa na vipindi vyao vya kutafakari peke yao, na hatimaye walitoa kazi bora na kupata cheo kikubwa.
   Tunaweza kufafanua methali kama misemo inatumika katika nchi au utamaduni fulani. Ni maneno mafupi yenye busara na hutoa ushauri na vile vile kuongeza wazo kuhusiana na maisha ya kila siku. Kwa kweli, ili kufahamu kwa kina mila na desturi za kitamaduni, ni vizuri warejelee methali kwani zinaweza kuwa na maana pana ndani. 
Kihistoria, methali "Still waters run deep" (Maji yalotulia ndo yenye kina kirefu/Usicheze maji yanayosimama) inatoka Kilatini cha kale. Ilipata umaarufu baada ya Shakespeare kuitumia katika tamthilia yake ya Henry VI mwaka 1590. Alisema:
"Maji hutulia pale ambapo mto una kina kirefu."

Tunatambua kwamba, mara nyingi watu hatari zaidi walio na roho mbaya hupanga hatua zao na kuchukua hatua kwa wakati ambao wengine hatarajii. Ndio maana usaliti hutoka kwa watu ambao hatutarajii [kitu kama hicho] kutoka kwao. Kwa hiyo ni muhimu kwa mtu kuchukua si tu yale yanayokutana na macho bali pia kuchukua tahadhari hasa kutoka kwa watu ambao hawalipizi kisasi mara tu baada ya kukasirishwa au kukabiliwa.
   Albert Einstein licha ya tabia yake ya kujittenga, yeye anajulikana sana kwa kubuni nadharia yake ya relativity ambayo ilileta mapinduzi katika uelewa wetu wa nafasi ya nje, wakati, na kanimvutano (gravity).
   Kwa kumalizia, ni muhimu sana kutofikia hitimisho [haraka] kwa sababu sura hudanganya na kuna mengi ya kujua na kugundua kuliko macho yanavyoweza kuona.
...
Updated 5mo ago
by
"na Ibrahim Nyanda
🏆 Shindano la Insha ya Methali
“Ni kwa nini kijiji chetu hakina maendeleo ukilinganisha na vijiji vingine vinavyotuzunguka? Vijana wengi kutoka vijiji vingine wa umri wetu wamesoma na wengine wana kazi zao za maana huko mjini. Pamoja na kwamba kuna shule kijijini kwetu lakini vijana hatufanyi vizuri shuleni na hata walimu wanapoajiriwa hawakai muda mrefu wanahama. Kuna nini hapa Bombambili?" Haya ni maswali ambayo kijana Akilimali alimwuliza rafiki yake Manase wakiwa machungani wakilisha ng’ombe. 

Mara baada ya swali hili Manase alionekana amezama katika wimbi kubwa la mawazo na mara baada ya kufikiri kwa muda alimgeukia rafiki yake Akilimali na kumtazama kwa kina kiaha akamwuliza, “Unaamini kuhusu ushirikina” Akilimali alijibu kwa kutikisa kichwa kuashiria kukubaliana na swali aliloulizwa na kisha akasema “Naamini kwani mara kadhaa nimekua nikiona watu wakienda kwa waganga na wengine wanapopitia magumu huamini wamerogwa, si unakumbuka juzi bibi Andunje tulivyoambiwa kuwa amekutwa juu ya paa la mzee Masanja uchi wa mnyama akiwanga, sasa mpaka hapo naachaje kuamini mshikaji wangu” 

Manase alimwangalia Akilimali kwa makini kisha akamwambia, "Nataka nikueleze siri moja ambayo huwezi amini……. hivi unajua kama mama yako na dada yako ni wachawi?” Akilimali alibaki ameduwaa mithili ya mjusi aloyebanwa na mlango halafu akiwa amefura kwa hasira akamwambia Manase “Aisee mwanangu usianze kuniletea habari zako za udwanzi hapa, tena koma kabisa kumwambia mama yangu mchawi vinginevyo ntakuja kukufanyia kitu mbaya hutokuja kuamini macho yako, ohoooo!!” 

Manase alimtuliza rafiki ake Akilimali halafu akamwambia, “Ngoja niwarudishe ng’ombe jirani afu nikupe mchapo mzima ulivyo, najua utanielewa we punguza jaziba kwanza” 

Mara baada ya kurudisha mifugo jirani Manase akaanza kumweleza Akilimali, “Rafiki angu nataka nikupe siri hii ambayo nimekaa nayo kwa muda mrefu, chochote unachokiona hapa hata kutokuwepo kwa naendeleo kijijini ni kwa sababu ya ushirikina, kila siku mama yako na dada yako huwa ninawaona wakija nyumbani wamepanda fisi wakimpitia mama kwenda kuwanga…..” Manase alitulia kidogo halafu akaendelea 

“Huwezi kuamini kwani hata mimj nilikua siamini mpaka nilipopakwa dawa na kuwaona, nitakupa hiyo dawa utapaka machoni na utakuja kunipa majibu kesho.” 

Mara baada ya mlo wa usiku Akilimali alikua ameketi akiota moto nje ya nyumba yao ya udongo iliyoezekwa kwa nyasi wakati huo mama yake na dada yake wakiwa ndani na yeye akiwa na baba yake pale nje. Alipaka ile dawa kama alivyoelekezwa na baada ya dakika kumi alimwona dada yake na mama yake wamepanda juu ya fisi mithili ya pikipiki tayari kwa safari ya kwenda kuwanga. 

“Nisamehe sana rafiki angu, ilikua ni hasira tu” aliongea maneno haya Akilimali huku akilengwa na machozi, 

“Mimi nilijua, sasa unavyoona kijijj chetu hakiendelei hata mama yako pia na dada yako wanahusika, inaumiza sana kila mwanakijiji anayetaka kuleta maendeleo anaishia kufa, lazima kuna siku watakuja kuumbuka kama ilivyokua kwa bibi Andunje” 

“Nina uhakika hata baba yako hajui kama mama yako na dada yako ni wachawi na kila siku huwa wanaenda kuwanga na ninyi kuwaachia mauzauza mkijua wapo, nenda kampake baba yako hiyo dawa alafu utanipa majibu” alieleza Manase 

Jioni kwa siri Akilimali alimweleza baba yake kuwa dada yake na mama yake ni wachawi kitu ambacho alipinga vikali. 

“Mama leo baba anatuona, angalia anvyotutumbulia macho” dada yake na Akilimali alimwabia mama yake wakiwa juu ya fisi kama ilivyo ada wakati baba yake na kaka yake wakiwa nje wanaota moto kama ilivyo kawaida yao. 

“Sidhani kama anatuona, hebu geuza fisi tuwe kama tunawaelekea wao” ailisema mana yake na Akilimali.

Akilimali anasema hiyo ndiyo ilikua siku ya mwisho kumwona baba yake kwani baada ya kuona fisi aliyewabeba mke wake na binti yake alitimua mbio kama anashundana mashindano ya mbio za mita mia. Ama kweli usilolijua ni kama usiku wa giza, Akilimali alibaki haamini kama kwa muda wote huo ameishi na mama yake na dada yake bila kujua kuwa ni wachawi. 
...
What one person throws away may be useful and valuable to someone else.

This saying is often used to describe either the diversity of human preferences or to express optimism that humans are quite creative when it comes to repurposing or recycling what other people throw away.

For example, entrepreneur Gibson Kiwago, founder of WAGA Tanzania, recycles old laptop batteries to power homes and businesses in Tanzanzia. Check out our E-Waste Reading List!

The notion that people subjectively assess quality has been around a long time. The saying derives from a 17th century proverb:
One man's meat is another man's poison.

Have you ever seen value in something that someone else threw away?
...
Updated 5mo ago
by