You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs

Mtoto akilia wembe, mpe

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
0
Updated 5mo ago
by
Habari zenu wapenzi wa lugha na hekima! Karibuni tena katika kipindi chetu cha leo cha Methali! Methali ya leo ni “Mtoto akilia wembe, mpe.” Je, unaijua? Kwa walezi wengi, inaweza kuonewa… kali sana, au sivyo? Ina maana gani kwako? Je, unakubaliana nayo? Tushirikiane mawazo. 

Nikisikia nitasahau, nikiona nitakumbuka, nikifanya nitaelewa.
-Mwalimu Amos 

Mtoto akitaka wembe, basi mpe ili aelewe kwanini alionywa dhidi ya kucheza nao. Methali hii inaonyesha umuhimu wa kuwapa watu nafasi za kujifunza kutokana na uzoefu wao wenyewe, hata kama wanaweza kuumiwa (kidogo). Vilevile, hata ukikataa kumpa, labda hatatiii na atacheza nao ukiwa nje. Methali hii inaweza kutumika pia kama onyo kwa mtu anayepuuza ushauri au kusisitiza njia yake. Ingawa ni muhimu kusikiliza ushauri na maonyo kutoka kwa wengine, wakati mwingine tunahitaji kuona matokeo ya vitendo vyetu wenyewe ili kuelewa madhara yake. 

Adhabu ya Asili  (Natural Consequences)

Katika eneo la malezi, methali hii inafundisha kanuni ya Natural Consequences (Adhabu Halisi au Adhabu ya Asili). Adhabu ya asili ni matokeo yatakayokuja kwa sababu ya tabia ya mtoto mwenyewe. Tofauti na adhabu ya kutolewa au adhabu ya viboko, adhabu ya asili hujitokeza bila mlezi kujiingilia. Kwa mfano, fikiria kama mwanako amesahau daftari yake nyumbani. Ungefanyaje? Wazazi wengine wanajibu “Singefanya chochote, maana atahitaji kueleza kwa mwalimu wake.” Wengine wanasema “Ningekimbia shuleni ili kumletea daftari, halafu jioni ningempa adhabu.” Ipi bora?  Jibuni hapo chini… 

Swali: Je, mtoto akilia nyoka utampa?

Sawa tumekubaliana mtoto akilia wembe, mpe. Lakini… fikiria kama mtoto analia kitu cha hatari zaidi— je utakubali? Yesu aliwauliza wazazi: “Mtoto akiomba samaki, je, atampa nyoka?” Akilia nyoka, utampa? Wembe unaweza kusababisha jeraha ndogo, lakini si hatari sana kama nyoka mwenye sumu. 
Wewe kama mzazi, utakubali kiasi gani cha hatari ili ajifunze mwenyewe? Kama anaomba kuacha masomo ili kucheza michezo za simu sikuzote? Kama anaomba kumwoa/kumwolewa na mtu ambaye haumwamini katika umri mdogo? Yaani pia kuna maamuzi muhimu ambayo watoto hawako tayari kujifanyia. 
Je wewe kama mzazi unawezaje kuamua au kutambua kama unapaswa kumwokoa / kumlinda mwanako, ama kama unapaswa kumwachia afunzwe na ulimwengu? Wazazi na walezi wote tunaomba maoni yenu!

Nyoka ana madhara.
-Mwalimu Shila  

Utekelezaji wa methali hii katika maisha ya kila siku

Elimu: Watu hukumbuka walichojifunza kwa vitendo kuliko walichoambiwa kwa maneno. Utafute nafasi za kutekeleza kile unachojifunza.
Malezi: Mpe mtoto uhuru na nafasi za kujifunza kupitia uzoefu. Usimtatulie kila jambo, na usiogope anapofeli, kama hakuna hatari wala madhara ya muda mrefu, maana kufeli ni nafasi ya kujifunza kwake.
Kusikiliza: Ukipuuza maonyo na shauri, usishangaye kuona madhara yaliyotabiriwa.
Details Picha hii imetengenezwa na akili bandia (AI)
Sources
Mathayo 7:10, Luka 11:11
Velten, C. (1903). Sitten und Gebräuche der Suaheli, nebst einem Anhang über Rechtsgewohnheiten der Suaheli. Vandenhoeck & Ruprecht. - Page 349

Loading...
Loading...
Login to view and post comments
It’s a simple and profound truth about human relationships: Making a promise means creating an expectation in others. When we fail to keep our promises, we damage our relationships and our reputation. Next time you make a promise, ask yourself, "Would I sign a contract that said this?"

French
Chose promise, chose due 
A thing promised is a thing owed. 
Russian:
Долг платежом красен, а займы отдачею. 
The beauty of a debt is its payment 
Alternative translation: A debt is beautiful when it is paid off, and loans when repaid.
Latin:
Pacta sunt servanda
Agreements must be kept (an important principle of international law)
Chinese
口說無憑
Spoken words are no guarantee.
English
Your word is your bond

What do you think? Is a promise as strong as a contract?
...
Updated 5mo ago
by
Have you ever noticed that time seems to pass more slowly when you are waiting for something? On the other hand, if you distract yourself with other engaging activities, time goes by quickly.

For example, if you're in a waiting room for a doctor, the wait will seem shorter if you check your phone or read a magazine, rather than just waiting for your name being called.

This proverb was attributed by Benjamin Franklin to Poor Richard's Almanac, however it doesn't actually appear there. Instead, Franklin used it in an essay on animal magnetism in 1785.

I was very Hungry; it was so late; “a watched pot is slow to boil,” as Poor Richard says.

...
Updated 5mo ago
by
Ustawi wa kiuchumi huenea na huwafikia raia wote wa nchi au eneo. Nchi haiwezi kufaidika bila raia wake wote kufaidika kwa namna moja au nyingine, kama vile baharini, maji yakijaa boti zote zitapanda, wimbi linalokuja litainua boti zote ziwe mitumbwi, jahazi, meli au mashua.

Msemo huo hutumiwa kumaanisha makundi yote yalinufaika kutokana na mabadiliko ya hali, hasa utitiri wa rasilimali, hata kama inaonekana kama zinawafikia matajiri wachache pekee. Nimesikia wafanyakazi wakiona wenzao wamepokea bonasi au kamisheni kubwa wanasema, "A rising tide lists all boats," ikimaanisha mauzo yakipanda, mapato ya kampuni yataongezeka na fursa kwa kampuni, na kwa hivyo, kwa wafanyikazi wote pia. Katika kesi hii, ni wazi wimbi halizinui boti zote kwa usawa au kiasi kilekile.

Wakosoaji wa methali hii wanaweza kulalamika kwamba methali hii inatumika pia ili kuhalalisha mpango au makubaliano yoyote hata kama yatawanufaisha wachache tu. Lakini kwa kawaida msemo huo husemwa  na viongozi kwa matumaini au kama pongezi.

Methali hiyo mara nyingi huhusishwa na John F. Kennedy rais wa Marekani, ambaye aliiitumia katika hotuba yake, mwaka wa 1963 akijitetea baada ya baada ya kukosolewa juu ya ujenzi wa bwawa ulitumia pesa nyingi sana (matumizi ya fujo). Mwandishi wa hotuba za Kennedy (aliyeitwa Ted Sorensen) alifichua kwamba Rais Kennedy alitumia methali hii baada ya kuisoma katika jarida la "New England Council."

Msemo karibu na huu ni "to grow the pie" yaani "kukuza keki" ambayo inamaanisha, kama keki ni kubwa zaidi, washiriki wote watapata keki zaidi hata kama uwiano/asilimia haibadiliki.

Je, unakubali kwamba ustawi mpana wa kiuchumi huwafikia wote?
...
Updated 5mo ago
by
Kadiri hamu ya kula inavyoongezeka, chakula kina ladha bora.

Methali hiyo ilionekana kwa mara ya kwanza katika kitabu cha Miguel de Cervantes Don Quixote, kilichochapishwa mwaka wa 1615 (katika Sehemu ya II, Sura ya V)

Mara nyingi wazazi husema hivi kwa watoto wao wanapokuwa walaji kwa fujo.
...
Updated 5mo ago
by