You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs

All that glitters is not gold

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
1
Updated 5mo ago
by
View this proverb in Swahili
Kila king’aacho si dhahabu
Once upon a time long ago, there was a beautiful, intelligent and kind young woman named Portia. Many men wanted to marry her and came to woo her. Portia’s father had died and left behind a will instructing that any suitor of Portia would have to choose among three caskets, one of gold, one of silver and one of lead. Only the suitor who chose correctly would be allowed to marry Portia and inherit all her father’s wealth. One day, the Prince of Morocco came to woo Portia.

The Merchant of Venice

Watch ▶️ on YouTube 

Portia: Go draw aside the curtains and discover
The several caskets to this noble prince.
Now make your choice.

Prince of Morocco: The first, of gold, who this inscription bears,
'Who chooseth me shall gain what many men desire;'
 The second, silver, which this promise carries,
 'Who chooseth me shall get as much as he deserves;'
 This third, dull lead, with warning all as blunt,
 'Who chooseth me must give and hazard all he hath.'
How shall I know if I do choose the right?

Portia: The one of them contains my picture, prince:
 If you choose that, then I am yours withal.

Prince of Morocco: Some god direct my judgment! Let me see;
 I will survey the inscriptions back again.
 What says this leaden casket?
 'Who chooseth me must give and hazard all he hath.'
 Must give: for what? for lead? hazard for lead?
 This casket threatens. Men that hazard all
 Do it in hope of fair advantages:
 A golden mind stoops not to shows of dross;
 I'll then nor give nor hazard aught for lead.
 What says the silver with her virgin hue?
 'Who chooseth me shall get as much as he deserves.'
 As much as he deserves! Pause there, Morocco,
 And weigh thy value with an even hand:
 If thou be'st rated by thy estimation,
 Thou dost deserve enough; and yet enough
 May not extend so far as to the lady:
 And yet to be afeard of my deserving
 Were but a weak disabling of myself.
 As much as I deserve! Why, that's the lady:
 I do in birth deserve her, and in fortunes,
 In graces and in qualities of breeding;
 But more than these, in love I do deserve.
 What if I stray'd no further, but chose here?
 Let's see once more this saying graved in gold
 'Who chooseth me shall gain what many men desire.'
 Why, that's the lady; all the world desires her;
 From the four corners of the earth they come,
 To kiss this shrine, this mortal-breathing saint:
 The Hyrcanian deserts and the vasty wilds
 Of wide Arabia are as thoroughfares now
 For princes to come view fair Portia:
 The watery kingdom, whose ambitious head
 Spits in the face of heaven, is no bar
 To stop the foreign spirits, but they come,
 As o'er a brook, to see fair Portia.
 One of these three contains her heavenly picture.
 Is't like that lead contains her? 'Twere damnation
 To think so base a thought: it were too gross
 To rib her cerecloth in the obscure grave.
 Or shall I think in silver she's immured,
 Being ten times undervalued to tried gold?
 O sinful thought! Never so rich a gem
 Was set in worse than gold. They have in England
 A coin that bears the figure of an angel
 Stamped in gold, but that's insculp'd upon;
 But here an angel in a golden bed
 Lies all within. Deliver me the key:
 Here do I choose, and thrive I as I may!

Portia: There, take it, prince; and if my form lie there,
 Then I am yours.

[He unlocks the golden casket]
Prince of Morocco: O hell! what have we here?
 A carrion Death, within whose empty eye
 There is a written scroll! I'll read the writing.
 [Reads]
All that glitters is not gold;
Often have you heard that told:
Many a man his life hath sold
But my outside to behold:
Gilded tombs do worms enfold.
Had you been as wise as bold,
Young in limbs, in judgment old,
Your answer had not been inscroll'd:
Fare you well; your suit is cold.
 Cold, indeed; and labour lost:
 Then, farewell, heat, and welcome, frost!
 Portia, adieu. I have too grieved a heart
 To take a tedious leave: thus losers part.
 [Exit with his train.

- From The Merchant of Venice by William Shakespeare, Act II Scene 7
Sources
Watch ▶️
The Merchant of Venice, Act II Scene 7 on YouTube
Ken Nwosu as the Prince of Morocco and Patsy Ferran as Portia, Directed by Polly Findlay, 2015 RSC
https://youtu.be/J9q7h9b-KWs?t=40m25s
Start time: 40m 25s
End time: 44m 37s

Old version:
Joan Plowright as Portia, Stephen Greif as the Prince of Morocco, Directed by Laurence Olivier, 1973
https://youtu.be/fJDg4ITyJIc?t=35m13s

Image: made with AI, CC-BY Maktaba.org 
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
na Rose Mwanri 🇹🇿 
🏆 Shindano la Insha ya Methali 
🥈 Mshindi wa Pili 

Akiba Haiozi

Methali ni usemi wa kimafumbo unaotumika katika jamii. Maneno katika methali huwa na maana ya ziada na methali huwa na pande mbili. Upande wa kwanza hutoa wazo na upande wa pili humalizia wazo. Akiba haiozi ni miongoni mwa methali za kiswahili inayotumika sana katika jamii za kiafrika na kwa watumiaji wa lugha ya kiswahili duniani, ikiwa na lengo la kuwaasa watu juu ya umuhimu wa kujiwekea akiba.

 Dhima ya methali hii ni kutusisitiza sisi wanajamii kujianda vema na maisha ya leo pamoja na kesho huku tukiwa tayari kuzikabili changamoto mbalimbali za maisha.

 Methali hii hutuonyesha ni kawaida mwanadamu kupatwa na dharura mbalimbali katika maisha ya kila siku. Mfano kupatwa na maradhi, ajali, au hata kifo. Pale unapokuwa na akiba uliyojiwekea itakusaidia wakati umepatwa na changamoto ya ghafla ambayo hukuitarajia.

 Faida nyingine ya kuweka akiba ni kuboresha maisha. Cha kwanza nashauri tuwe na utaratibu wa kuweka akiba mara kwa mara ili kuweza kuboresha maisha yetu kwa ujumla. Tunavyozidi kuweka akiba ndivyo ambavyo akiba hiyo inaweza kutusaidia kuboresha makazi yetu na miundombinu kwa ujumla ndani ya jamii zetu. Mfano mzuri ni wazazi ambao akiba wanazoziweka huwasaidia kulipa karo za shule pamoja na kununua vifa mbalimbali vya shulena hata gharama zingine zinazojitokeza kwa wakati huo.

 Methali hii pia inatukumbusha kuwa kadri tunavyozidi kuweka akiba ndivyo tunavyokuza hazina yetu. Swa na ile methali inayosema “ Haba na haba hujaza kibaba” ukichambua methali hizi zinaendana maana na utagundua ni ukumbusho mkubwa kwetu kuhusu ujenzi wa hatma njema ya jamii yetu ya sasa na baadae. Kwa kuwa zinatuhimiza kuwekeza kwa kila chumo tulipatalo. Tunakuza hazina kwa kuwa kile tunachoweka akiba kipo kwaajili yetu.

 Chukua nafasi kujiuliza, ni mara ngapi umepatwa na changamoto na akiba ndiyo ikaokoa jahazi, ni mambo mangapi yametokea bila taarifa na akiba ndiyo imetumika kuweka mambo sawa. Naamini sote tunapaswa kuweka akiba bila kujali kipato ni kikubwa au kidogo. Mfano unaweza kuanza kuweka akiba kidogo kidogo kutokana na kile unachokipata na kufikia muda Fulani utakuwa na akiba kubwa.

 Vilevile methali hii inasaidia kukuza maarifa kwa mtu mmoja mmoja na jamii hasa pale ambapo pamekuwepo na tofauti ya uhifadhi wa akiba kutoka kizazi kimoja kwenda kingine. Hapo zamani tunaambiwa watu walikuwa wanahifadhi akiba zao kwa kuchimba chini ya ardhi, kuweka chini ya kitanda au hata sehemu zingine ambazo wao waliamini ni salama. Leo hii watu hawatumii sana njia za kienyeji kuweka akiba zao. Ukija kwenye fedha zipo benki zenye mifumo thabiti na salama katika kuhifadhi fedha. Kwa upande wa akiba ya mazao pia zipo njia salama za kuhifadhi tena hata kwa muda mrefu bila kuharibika. Kwa hakika akiba haiozi.

 Waswahili tunasema “akiba haiozi”, “haba na haba hujaza kibaba” ikimaanisha kwamba akiba yaweza kuonekana ndogo ila kadri inavyoongezeka ndivyo inavyokuwa kubwa. Kinyume chake tunaambiwa “Chovya chovya humaliza buyu la asali”, “Bandu bandu humaliza gogo”. Tukikumbushwa kuwa vile tunavyochukua akiba zetu kidogo kidogo bila sababu ya msingi ndivyo ambavyo iko siku tutahamaki na kuona akiba imeisha bila kuona kitu cha maana kilichofanyika. Tukumbuke “mali bila daftari huisha bila habari”, tuangalie mfano wa shairi hili linalotusisitiza kuhusu kuweka akiba.

Akiba kweli hazina, haijawahi saliti,
Kwetu ni muhimu sana, hutubeba kwa nyakati,
Kipindi kweli hatuna, inasimama kwa dhati,
Sote tuweke akiba, akiba ni mkombozi.

 Kwa hakika ni dhahiri yatupasa kutunza vitu vyetu vizuri na rasilimali tulizonazo kwa kuweka akiba ili tuweze kujinusuru pale ambapo tunapokumbwa na changamoto za kushtukiza kwa ajili ya maisha yetu ya sasa na ya baadae.

...
This proverb means that we often get treated the same way we treat others. It is usually negatively, as a warning, or when a person who acted immorally gets their comeuppance. It could also be used as a promise of blessings to those who do good.  A third possible meaning is that Often compared to the Hindu doctrine of karma, the exact origin of the proverb is uncertain, but it seems to have emerged in the US in middle of the last century.

Related proverbs and quotes:
Shakespeare 
We still have judgment here; that we but teach
Bloody instructions, which, being taught, return
To plague the inventor: this even-handed justice
Commends the ingredients of our poison'd chalice
To our own lips.  (Macbeth Act I, Scene 7
Bible:
As you sow, so shall you reap (Galatians 6:7)
Chinese:
善有善報,惡有惡報
Good is rewarded with good, and evil with evil.
German
Wie man in den Wald hineinruft, so schallt es heraus
What you shout into the forest, will echo out again

...
Updated 5mo ago
by

Ufafanuzi


Methali hii ya Kiingereza inatafsirika pia kama "Kalamu ina nguvu kuliko upanga au jambia" au " Kalamu ni kali kuliko upanga." Katika methali hii, jambia au upanga unaashiria nguvu na ukatili, na maana ya kalamu ni maneno. Ingawa upanga unaweza kushinda kwa nguvu, kalamu inaweza kuwashawishi, kuwahamasisha, na kuwaelimisha watu. Sio kila mtu ana silaha za kuwalazimisha watu wengine kufanya kile anachotaka, lakini kila mtu ana uwezo wa kubadilisha ulimwengu kupitia kile anachofikiria, kusema na kuandika kwa maneno. 

Silaha za siku hizi ni kalamu na karatasi.
 - Methali ya Kiswahili

Methali hii ni kweli kwa sababu mara nyingi maneno huchochea na kudhibiti jinsi watu wanavyotumia nguvu na silaha zao. Kwa mfano, kupitia sheria, maneno ya viongozi, mahakimu na majaji yana uwezo wa kuwafunga watu gerezani au hata kuwaua. Kutoa hotuba ya moto kwa umati wa watu wenye hasira kunaweza kuleta ghasia kali na madhara mengine (ona Juliasi Kaizari).

"Ukinipa picha, nitakupa vita."
- William Randolph Hearst
(Mwandishi wa habari na mchapishaji wa magazeti, Marekani)

Lakini pia, methali hiyo inatukumbusha nguvu ya upinzani usio na vurugu kwenye kuleta mabadiliko ya kudumu, kanuni iliyotetewa na kuonyeshwa na watu kama Mahatma Gandhi, Martin Luther King, na Nelson Mandela.  Angalia pia: Insha ya "Civil Disobedience"  na Henry David Thoreau, pamoja na Tamthilia mashuhuri ya "Antigone" na Sophocles.

Chimbuko


Nukuu hii ya "kalamu ina nguvu kuliko upanga" ilipata umaarufu kupitia tamthilia ya "Richelieu: au The Conspiracy"  na Edward Bulwer-Lytton (mwaka wa 1839, ukurasa wa 47). Lakini hakika wazo lilikuwepo kabla.

Wengine wanasema chimbuko halisi la methali hii ni Hadithi ya Ahikar. Kitabu hiki kiliandikwa takriban miaka 600 kabla ya kristu, na ni chimbuko la methali zingine kama "Ndege mkononi ana thamani ya wawili mtini"). Katika toleo letu, mfasiri hakuweza kusoma maandishi kutokana na hali ya karatasi, na maneno yalikatika. (Ukurasa 171/274
Dhibiti kinywa chako kwa uangalifu ...[ILIKATA]... na ufanye moyo wako kuwa mzito(?), kwa maana neno linalosemwa ni kama ndege, naye alitamkaye ni kama mtu asiye na  ...[ILIKATA]... ufundi wa maneno una nguvu zaidi kuliko ufundi wa  ...[ILIKATA]...
- Hadithi ya Ahikar, Ukurasa wa 171/274
Je, hili ndilo chimbuko halisi la methali hii, miaka zaidi ya 2,500 iliyopita? Muwe majaji...

Chanzo karibu na methali hii pia kinaonekana katika Agano la Kale:
Kwa maana neno la Mungu ni hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili.
Waebrania 4:12, Biblia

Na vilevile katika Shakespeare: 
Wengi wanaovaa panga huogopa kalamu.
-William Shakespeare
Tamthilia ya Hamlet, Sehemu ya 2, Onyesho la II (ukurasa wa 59)

 Je, unakubali kalamu hushinda jambia? Toa maoni yako hapo chini!
...

CC BY Unaruhusiwa kunakili & kusambaza mchoro huu na makala hii bila idhini, ukitaja tu chanzo (www.maktaba.org)

Updated 5mo ago
by
Watu wengi wanaogopa kuuliza maswali kwa sababu wanahofia kuonwa mjinga. Lakini kuuliza maswali ni njia bora ya kujifunza kutoka kwa wengine. 

Pia kuuliza maswali husaidia wenzako. Je umewahi kusita kuuliza swali kwani ulidhani wengine wameshaelewa... lakini baadaye uligundua hawakuelewa pia? 

Kiingereza
There's no such thing as a stupid question
...
Updated 5mo ago
by