Ukitaka kwenda haraka, nenda peke yako, ukitaka kwenda mbali, nenda na wenzako
Rome ne fu[t] pas faite toute en un jour
Kutoka kitabu cha Li Proverbe au Vilain kilichochapishwa takriban mwaka wa 1190
Kifaransa cha kisasa: Rome ne s'est pas faite en un jour
Maana yake: Roma haikujengwa kwa siku moja
冰凍三尺,非一日之寒
Mita ya barafu sio kwa sababu ya siku moja ya baridi
Chan ann leis a’ chiad bhuille a thuiteas a’ chraobh
Sio pigo la kwanza linaloangusha mti
Picha: Shukran kwa Zamani Project waliounda ziara ya mtandaoni ya Kilwa Kisiwani!
Mtaka cha mvunguni sharti ainame
Mulla [Nasreddin] alikuwa amepoteza pete yake sebuleni. Aliitafuta kwa muda, lakini kwa kuwa hakuipata, alitoka nje hadi uani na kuanza kuchungulia pale. Mkewe, ambaye aliona alichokifanya, akamwuliza: “Mulla, umepoteza pete yako sebuleni , kwa nini unaitafuta uani?” Mulla alishika ndevu zake akisema: “Chumbani kuna giza na sioni vizuri. Nilitoka nje kwenda uani ili kutafuta pete yangu kwa sababu kuna mwanga mwingi zaidi hapa.
[Afisa wa polisi alikutana na mwanamume akipapasa-papasa akipiga magoti] “Nilipoteza noti ya $2 kwenye barabara ya Atlantic,” kasema mwanamume huyo. "Nini kile?" aliuliza afisa aliyeshangaa. "Umepoteza notiya $2 kwenye barabara ya Atlantic? Kwa nini basi unaitafuta hapa Copley Square?" “Kwa sababu,” akasema akiendelea na utafutaji wake, “mwanga ni bora hapa."
Mchoro huu umetengenezwa kwa kutumia Akili Bandia (AI). Unafikiriaje?
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana.’
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho.’
‘Anichaguaye mimi itambidi atoe, na pia ahatarishe chochote alicho nacho.’
‘Anichaguaye mimi itambidid atoe na pia ahatarishe cho chote alicho nacho.’
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho’.
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana!’
Kila kitu king’aacho usidhani ni dhahabu,
umekisikia hicho ni kiambo cha mababu.
Kuniona kwa nje tu, wengi wameuza utu;
Makaburi ya dhahabu yana mafunza ajabu.
Ungekuwa na werevu ulivyo na ushupavu,
kijana kiwiliwili na mzee kwa akili,
usingelistahili kulipewa jibu hili:
Basi buriani dawa; pposa umefarikiwa.