Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Fungua akaunti mpya

Taarifa
Majadiliano
Methali
Akiba Haiozi
ili kupiga kura
Kura
60
View this proverb in English
Savings don't rot
na Rose Mwanri đŸ‡č🇿 
🏆 Shindano la Insha ya Methali 
đŸ„ˆ Mshindi wa Pili 

Akiba Haiozi

Methali ni usemi wa kimafumbo unaotumika katika jamii. Maneno katika methali huwa na maana ya ziada na methali huwa na pande mbili. Upande wa kwanza hutoa wazo na upande wa pili humalizia wazo. Akiba haiozi ni miongoni mwa methali za kiswahili inayotumika sana katika jamii za kiafrika na kwa watumiaji wa lugha ya kiswahili duniani, ikiwa na lengo la kuwaasa watu juu ya umuhimu wa kujiwekea akiba.

 Dhima ya methali hii ni kutusisitiza sisi wanajamii kujianda vema na maisha ya leo pamoja na kesho huku tukiwa tayari kuzikabili changamoto mbalimbali za maisha.

 Methali hii hutuonyesha ni kawaida mwanadamu kupatwa na dharura mbalimbali katika maisha ya kila siku. Mfano kupatwa na maradhi, ajali, au hata kifo. Pale unapokuwa na akiba uliyojiwekea itakusaidia wakati umepatwa na changamoto ya ghafla ambayo hukuitarajia.

 Faida nyingine ya kuweka akiba ni kuboresha maisha. Cha kwanza nashauri tuwe na utaratibu wa kuweka akiba mara kwa mara ili kuweza kuboresha maisha yetu kwa ujumla. Tunavyozidi kuweka akiba ndivyo ambavyo akiba hiyo inaweza kutusaidia kuboresha makazi yetu na miundombinu kwa ujumla ndani ya jamii zetu. Mfano mzuri ni wazazi ambao akiba wanazoziweka huwasaidia kulipa karo za shule pamoja na kununua vifa mbalimbali vya shulena hata gharama zingine zinazojitokeza kwa wakati huo.

 Methali hii pia inatukumbusha kuwa kadri tunavyozidi kuweka akiba ndivyo tunavyokuza hazina yetu. Swa na ile methali inayosema “ Haba na haba hujaza kibaba” ukichambua methali hizi zinaendana maana na utagundua ni ukumbusho mkubwa kwetu kuhusu ujenzi wa hatma njema ya jamii yetu ya sasa na baadae. Kwa kuwa zinatuhimiza kuwekeza kwa kila chumo tulipatalo. Tunakuza hazina kwa kuwa kile tunachoweka akiba kipo kwaajili yetu.

 Chukua nafasi kujiuliza, ni mara ngapi umepatwa na changamoto na akiba ndiyo ikaokoa jahazi, ni mambo mangapi yametokea bila taarifa na akiba ndiyo imetumika kuweka mambo sawa. Naamini sote tunapaswa kuweka akiba bila kujali kipato ni kikubwa au kidogo. Mfano unaweza kuanza kuweka akiba kidogo kidogo kutokana na kile unachokipata na kufikia muda Fulani utakuwa na akiba kubwa.

 Vilevile methali hii inasaidia kukuza maarifa kwa mtu mmoja mmoja na jamii hasa pale ambapo pamekuwepo na tofauti ya uhifadhi wa akiba kutoka kizazi kimoja kwenda kingine. Hapo zamani tunaambiwa watu walikuwa wanahifadhi akiba zao kwa kuchimba chini ya ardhi, kuweka chini ya kitanda au hata sehemu zingine ambazo wao waliamini ni salama. Leo hii watu hawatumii sana njia za kienyeji kuweka akiba zao. Ukija kwenye fedha zipo benki zenye mifumo thabiti na salama katika kuhifadhi fedha. Kwa upande wa akiba ya mazao pia zipo njia salama za kuhifadhi tena hata kwa muda mrefu bila kuharibika. Kwa hakika akiba haiozi.

 Waswahili tunasema “akiba haiozi”, “haba na haba hujaza kibaba” ikimaanisha kwamba akiba yaweza kuonekana ndogo ila kadri inavyoongezeka ndivyo inavyokuwa kubwa. Kinyume chake tunaambiwa “Chovya chovya humaliza buyu la asali”, “Bandu bandu humaliza gogo”. Tukikumbushwa kuwa vile tunavyochukua akiba zetu kidogo kidogo bila sababu ya msingi ndivyo ambavyo iko siku tutahamaki na kuona akiba imeisha bila kuona kitu cha maana kilichofanyika. Tukumbuke “mali bila daftari huisha bila habari”, tuangalie mfano wa shairi hili linalotusisitiza kuhusu kuweka akiba.

Akiba kweli hazina, haijawahi saliti,
Kwetu ni muhimu sana, hutubeba kwa nyakati,
Kipindi kweli hatuna, inasimama kwa dhati,
Sote tuweke akiba, akiba ni mkombozi.

 Kwa hakika ni dhahiri yatupasa kutunza vitu vyetu vizuri na rasilimali tulizonazo kwa kuweka akiba ili tuweze kujinusuru pale ambapo tunapokumbwa na changamoto za kushtukiza kwa ajili ya maisha yetu ya sasa na ya baadae.

Marejeleo

Juu ya Insha hii

Insha hii ilishinda nafasi ya pili đŸ„ˆ katika Shindano la Methali ya Insha la Maktaba.org 🏆 7/7/2023
Rose Mwanri ni mwalimu Mtanzania đŸ‡č🇿 

Hakimiliki

Creative Commons Attribution (CC BY 4.0)
na Rose Mwanri
Ilichapishwa na Maktaba.org
Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org

Related on Maktaba.org 


Loading...
Loading...
Ingia akaunti yako ili kuona na kutoa maoni
Many people are afraid to ask questions because they don't want to be seen as stupid. But asking questions is the best way to learn from others.

Asking questions also helps others around you. Have you ever hesitated to ask a question because you thought others already understood... but later you realized they didn't either? 

This proverb is similar to the English saying, “There's no such thing as a stupid question.”
...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
Tofautisha na linganisha matunda na pipi. Matunda yameiva, yana ladha halisi, yamejaa virutubisho na vitamini -- kweli yanajiuza yenyewe.

Kwa upande mwingine, mfuko wa pipi unalia “nisikilize!”, kwa rangi kali, na kauli mbiu zinazolipuka *BOOM*! Lakini chini au nyuma ya kinachong'aa, tunajua kwa kkweli pipi ni sukari tupu tu yenye rangi na ladha bandia ya matunda.

Kama nyani, binadamu hupenda matunda kwa sababu yanatupatia nishati pamoja na lishe na virutubisho. Pipi hutoa nishati bila lishe halisi (Kalori tupu). Pipi huiga tunda. Usidanganywe!

Kizuri hakihitaji kutangazwa, maana ubora hujieleza yenyewe. Kama wachumi wasemavyo, “demand” inazidi “supply”. Matangazo yanaweza kutuahidi furaha, uzuri, upendo, mali au heshima. Lakini jiulize, je, inawezekana kwa kweli? Coca-Cola sio dawa ya upendo.

Methali hii inatukumbusha thamani ya ubora wa kweli kuliko muonekeano maridadi. Methali hii hutumika wakati msemaji ana mashaka juu ya mtu anayejisifu au kujivunia kupita kiasi.

Tuwe kama kikapu cha matunda: mwazi na mwema. Sifa hizi zitawavuta wengine kwako — angalau wao wanaoelewa kwamba “Chema chajiuza, kibaya chajitembeza!”

Methali zinazohusiana:
Vingaravyo vyote si dhahabu

Don’t judge ya book by it’s cover
Usihukumu kitabu kwa kava yake (muonekeno)

Appearances are deceptive
Maonekano hudanganya
 
高ć¶șăźèŠ±
Hana yori dango
Chakula [ni bora] kuliko maua
...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by

Meaning 


In this proverb, the sword signifies force and violence, and the pen stands for words. While the sword can conquer with force, the pen can persuade, inspire, enlighten and motivate people. Not everyone has weapons to force other people to do what they want, but everyone has the power to influence the world through what they think, say and write with words.

Silaha za siku hizi ni kalamu na karatasi.
Today's weapons are pen and paper.
 - Swahili proverb

Part of the reason this proverb is true is that words often motivate and regulate how people use violence and force. For example, through law, the words of leaders, judges and juries have the power to jail people or even kill them. Making a fiery speech to an angry mob might cause a violent riot (see Julius Caesar). 

You furnish the pictures and I'll furnish the war.
- William Randolph Hearst

The proverb also reminds us of the power of nonviolent resistance to bring about lasting political change, a principle advocated and demonstrated by figures like Mahatma Gandhi, Martin Luther King, and Nelson Mandela. (Check out Henry David Thoreau's classic Essay, "Civil Disobedience" and Sophocles famous play, "Antigone")

Origin


The phrase "the pen is mightier than the sword" became popular after Edward Bulwer-Lytton used it in his 1839 play "Richelieu: Or the Conspiracy" (page 47).  But the idea likely originated much earlier.

Some sources attribute the proverb to the Story of Ahikar (which is also the source of the proverb "A bird in the hand is worth two in the bush"). In this edition, the translator was unable to decipher the damaged manuscript and left the sentence unfinished. (Page 171/274) 
(FRAGMENTS)
Watch carefully over thy mouth ...... and make thy heart slow(?), for the word spoken is like a bird, and he who utters it is like a man without ...
... the craft of the mouth is mightier than the craft of ...... 
Could this be the original source of the proverb from over 2500 years ago? You be the judge...

A similar phrase also appears in the Old Testament: 
For the word of God is quick, and powerful, and sharper than any two-edged sword.
Hebrews 4:12 (KJV)

And in Shakespeare:
 Many wearing rapiers are afraid of goosequills.
-William Shakespeare Hamlet Act 2, scene II (page 59)

Do you agree that the pen is mightier than the sword? Share your opinions below!

...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
by Magreth Lazaro Mafie đŸ‡č🇿
🏆 Proverb Essay Contest 
đŸ„‰ Third Place Winner
(English translation from Kiswahili)
How many times have you heard “Mchumia juani hulia kivulini” (One who works in the sun, eats in the shade). This is a Swahili (Bantu) proverb meant to encourage people in their everyday activities, to have faith that there will be a day when they will enjoy the fruits of their work.

This proverb gives people strength, diligence, heart, courage, hope and skill in working. The worker believes that hard work brings a good harvest that will allow him to relax in the shade as he eats the fruits of his labor. 

The following poem shows “One who works in the sun” in their daily responsibilities.
I fear neither sun nor rain, making my tomorrow
I fear neither injuries nor pain, because all are temporary
Scorching sun and work are my custom, so that happiness comes in life
The street vendor, the farmer, the [port boys] and their fisherman and the sun, in search of tomorrow
One who works in the sun, eats in the shade, I am still searching for shade.

It's noon, the sun overhead, in my head I have the harvest, sweat is dripping,
The sun has set now, the oar on the beach, exhausted in bed, nets in the sea,
At home on fourth street, captain of the family, may I pull happiness from hard labor
Now the sun is rising, walking the path to look for a bite,
One who works in the sun, eats in the shade, I am still searching for shade.

Once there was a farmer. He spent his whole life in agriculture. Thus his times for pleasure were few. People in his village called him a skilled farmer. He built a house by selling part of his crops, he educated his children through farming.

This farmer was a diligent man, he always learned the principles of being a good farmer, so as time went by, he harvested many crops from his fields. Many people were really amazed to see the big changes in his family. He made many investments in his village, the farms, houses, and shops, and many livestock came from his farm.

Many people came to take wisdom from the skilled farmer. He always told them "One who works in the sun, eats in the shade. The hoe has given me respect in the village, me and my family. My life now is going on a path of certainty, I am in the shade, enjoying the fruits of my labor in the sun. I, the son of that skilled farmer, am proud of my upbringing, and his responsibility, because work in the sun today has made us rest and eat in the shade. The true meaning of “he who works in the sun” can be seen in actions. Your diligence is your sun and the shade is the fruit of your diligence.

This story is complemented by the story of "Mabala the Farmer" by Richard S. Mabala (1989). Mabala was a port worker then he was demoted, so he chose to return to the village of Morogoro. Mabala was careless, drunk and obstinate. Mabala went to the farm with a gallon of booze, he drank it and went to sleep, when he woke up, he called out to his wife but there was no answer except the sound of the hoe tik-tok, tik-tok.

Mabala was obstinate, he watered the fields with sugar, thinking it was fertilizer, but in the end he changed to become a skilled farmer, becoming “one who works” in the sun so that his family could eat in the shade. Do you feel that Mabala is “one who works in the sun”? In the family or in the community, what’s your image of a skilled farmer?

In conclusion, this story on the proverb "Work in the sun, eat in the shade" shows us a good vision in everything we do in our daily lives. Also proverbs like "Subira yavuta kheri” (Patience brings blessings), "Mgaa na Upwa hali wali mkavu” (He who combs the beach at low tide doesn’t eat dry rice) all have similar themes; they exist to give the community strength and hope each task undertaken to pursue their goals.

...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by